96 - The Clot - Al-`Alaq
:1
Soma kwa jina la Mola wako Mlezi aliye umba,
:2
Amemuumba binaadamu kwa tone la damu,
:3
Soma! Na Mola wako Mlezi ni Karimu kushinda wote!
:4
Ambaye amefundisha kwa kalamu.
:5
Kamfundisha mtu aliyo kuwa hayajui.
:6
Kwani! Hakika mtu bila ya shaka huwa jeuri
:7
Akijiona katajirika.
:8
Hakika kwa Mola wako Mlezi ndio marejeo.
:9
Umemwona yule anaye mkataza
:10
Mja anapo sali?
:11
Umeona kama yeye yuko juu ya uwongofu?
:12
Au anaamrisha uchamngu?
:13
Umeona kama yeye akikanusha na anarudi nyuma?
:14
Hajui ya kwamba Mwenyezi Mungu anaona?
:15
Kwani! Kama haachi, tutamkokota kwa shungi la nywele!
:16
Shungi la uwongo, lenye makosa!
:17
Basi na awaite wenzake!
:18
Nasi tutawaita Mazabania!
:19
Hasha! Usimt'ii! Nawe sujudu na ujongee!