Maktaba yote ya Kiislamu

96 - The Clot - Al-`Alaq

:1

Soma kwa jina la Mola wako Mlezi aliye umba,

:2

Amemuumba binaadamu kwa tone la damu,

:3

Soma! Na Mola wako Mlezi ni Karimu kushinda wote!

:4

Ambaye amefundisha kwa kalamu.

:5

Kamfundisha mtu aliyo kuwa hayajui.

:6

Kwani! Hakika mtu bila ya shaka huwa jeuri

:7

Akijiona katajirika.

:8

Hakika kwa Mola wako Mlezi ndio marejeo.

:9

Umemwona yule anaye mkataza

:10

Mja anapo sali?

:11

Umeona kama yeye yuko juu ya uwongofu?

:12

Au anaamrisha uchamngu?

:13

Umeona kama yeye akikanusha na anarudi nyuma?

:14

Hajui ya kwamba Mwenyezi Mungu anaona?

:15

Kwani! Kama haachi, tutamkokota kwa shungi la nywele!

:16

Shungi la uwongo, lenye makosa!

:17

Basi na awaite wenzake!

:18

Nasi tutawaita Mazabania!

:19

Hasha! Usimt'ii! Nawe sujudu na ujongee!