1
Hakika Sisi tumeiteremsha Qur'ani katika Laylatul Qadri, Usiku wa Cheo Kitukufu.
2
Na nini kitacho kujuulisha nini Laylatul Qadri?
3
Laylatul Qadri ni bora kuliko miezi elfu.
4
Huteremka Malaika na Roho katika usiku huo kwa idhini ya Mola wao Mlezi kwa kila jambo.
5
Amani usiku huo mpaka mapambazuko ya alfajiri.