All Islam Directory
1

Hakika Sisi tumeiteremsha Qur'ani katika Laylatul Qadri, Usiku wa Cheo Kitukufu.

2

Na nini kitacho kujuulisha nini Laylatul Qadri?

3

Laylatul Qadri ni bora kuliko miezi elfu.

4

Huteremka Malaika na Roho katika usiku huo kwa idhini ya Mola wao Mlezi kwa kila jambo.

5

Amani usiku huo mpaka mapambazuko ya alfajiri.