Maktaba yote ya Kiislamu

1 - The Opener - Al-Fātiĥah

:1

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

:2

Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa viumbe vyote;

:3

Mwingi wa Rehema Mwenye Kurehemu;

:4

Mwenye Kumiliki Siku ya Malipo.

:5

Wewe tu tunakuabudu, na Wewe tu tunakuomba msaada.

:6

Tuongoe njia iliyo nyooka,

:7

Njia ya ulio waneemesha, siyo ya walio kasirikiwa, wala walio potea.