95 - The Fig - At-Tīn
:1
Naapa kwa tini na zaituni!
:2
Na kwa Mlima wa Sinai!
:3
Na kwa mji huu wenye amani!
:4
Bila ya shaka tumemuumba mtu kwa umbo lilio bora kabisa.
:5
Kisha tukamrudisha kuwa chini kuliko walio chini!
:6
Lakini wale walio amini na wakatenda mema, hao watapata ujira usio kwisha.
:7
Basi ni kipi baadaye kitacho kukukadhibishia malipo?
:8
Kwani Mwenyezi Mungu si muadilifu kuliko mahakimu wote?