Maktaba yote ya Kiislamu
1

Naapa kwa tini na zaituni!

2

Na kwa Mlima wa Sinai!

3

Na kwa mji huu wenye amani!

4

Bila ya shaka tumemuumba mtu kwa umbo lilio bora kabisa.

5

Kisha tukamrudisha kuwa chini kuliko walio chini!

6

Lakini wale walio amini na wakatenda mema, hao watapata ujira usio kwisha.

7

Basi ni kipi baadaye kitacho kukukadhibishia malipo?

8

Kwani Mwenyezi Mungu si muadilifu kuliko mahakimu wote?