Maktaba yote ya Kiislamu

95 - The Fig - At-Tīn

:1

Naapa kwa tini na zaituni!

:2

Na kwa Mlima wa Sinai!

:3

Na kwa mji huu wenye amani!

:4

Bila ya shaka tumemuumba mtu kwa umbo lilio bora kabisa.

:5

Kisha tukamrudisha kuwa chini kuliko walio chini!

:6

Lakini wale walio amini na wakatenda mema, hao watapata ujira usio kwisha.

:7

Basi ni kipi baadaye kitacho kukukadhibishia malipo?

:8

Kwani Mwenyezi Mungu si muadilifu kuliko mahakimu wote?