All Islam Directory
1

Hatukukunjulia kifua chako?

2

Na tukakuondolea mzigo wako,

3

Ulio vunja mgongo wako?

4

Na tukakunyanyulia utajo wako?

5

Basi kwa hakika pamoja na uzito upo wepesi,

6

Hakika pamoja na uzito upo wepesi.

7

Na ukipata faragha, fanya juhudi.

8

Na Mola wako Mlezi ndio mshughulikie.