1
Naapa kwa mchana!
2
Na kwa usiku unapo tanda!
3
Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukasirika nawe.
4
Na bila ya shaka wakati ujao utakuwa bora kwako kuliko ulio tangulia.
5
Na Mola wako Mlezi atakupa mpaka uridhike.
6
Kwani hakukukuta yatima akakupa makaazi?
7
Na akakukuta umepotea akakuongoa?
8
Akakukuta mhitaji akakutosheleza?
9
Basi yatima usimwonee!
10
Na anaye omba au kuuliza usimkaripie!
11
Na neema za Mola wako Mlezi zisimlie.