Maktaba yote ya Kiislamu

93 - The Morning Hours - Ađ-Đuĥaá

:1

Naapa kwa mchana!

:2

Na kwa usiku unapo tanda!

:3

Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukasirika nawe.

:4

Na bila ya shaka wakati ujao utakuwa bora kwako kuliko ulio tangulia.

:5

Na Mola wako Mlezi atakupa mpaka uridhike.

:6

Kwani hakukukuta yatima akakupa makaazi?

:7

Na akakukuta umepotea akakuongoa?

:8

Akakukuta mhitaji akakutosheleza?

:9

Basi yatima usimwonee!

:10

Na anaye omba au kuuliza usimkaripie!

:11

Na neema za Mola wako Mlezi zisimlie.