Maktaba yote ya Kiislamu
1

Naapa kwa mchana!

2

Na kwa usiku unapo tanda!

3

Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukasirika nawe.

4

Na bila ya shaka wakati ujao utakuwa bora kwako kuliko ulio tangulia.

5

Na Mola wako Mlezi atakupa mpaka uridhike.

6

Kwani hakukukuta yatima akakupa makaazi?

7

Na akakukuta umepotea akakuongoa?

8

Akakukuta mhitaji akakutosheleza?

9

Basi yatima usimwonee!

10

Na anaye omba au kuuliza usimkaripie!

11

Na neema za Mola wako Mlezi zisimlie.