Maktaba yote ya Kiislamu

92 - The Night - Al-Layl

:1

Naapa kwa usiku unapo funika!

:2

Na mchana unapo dhihiri!

:3

Na kwa Aliye umba dume na jike!

:4

Hakika juhudi zenu bila ya shaka ni mbali mbali.

:5

Ama mwenye kutoa na akamchamngu,

:6

Na akaliwafiki lilio jema,

:7

Tutamsahilishia yawe mepesi.

:8

Na ama mwenye kufanya ubakhili, na asiwe na haja ya wenzake,

:9

Na akakanusha lilio jema,

:10

Tutamsahilishia yawe mazito!

:11

Na mali yake yatamfaa nini atapo kuwa anadidimia?

:12

Hakika ni juu yetu kuonyesha uwongofu.

:13

Na hakika ni yetu Sisi Akhera na dunia.

:14

Basi nakuonyeni na Moto unao waka!

:15

Hatauingia ila mwovu kabisa!

:16

Anaye kadhibisha na kupa mgongo.

:17

Na mchamngu ataepushwa nao,

:18

Ambaye hutoa mali yake kwa ajili ya kujitakasa.

:19

Na wala si kwa kuwa yupo yeyote aliye mfanyia hisani ndio anamlipa.

:20

Ila ni kutaka radhi ya Mola wake Mlezi aliye juu kabisa.

:21

Naye atakuja ridhika!