91 - The Sun - Ash-Shams
:1
Naapa kwa jua na mwangaza wake!
:2
Na kwa mwezi unapo lifuatia!
:3
Na kwa mchana unapo lidhihirisha!
:4
Na kwa usiku unapo lifunika!
:5
Na kwa mbingu na kwa aliye ijenga!
:6
Na kwa ardhi na kwa aliye itandaza!
:7
Na kwa nafsi na kwa aliye itengeneza!
:8
Kisha akaifahamisha uovu wake na wema wake,
:9
Hakika amefanikiwa aliye itakasa,
:10
Na hakika amekhasiri aliye iviza.
:11
Kina Thamudi walikadhibisha kwa sababu ya upotofu wao,
:12
Alipo simama mwovu wao mkubwa,
:13
Hapo Mtume wa Mwenyezi Mungu alipo waambia: Huyu ni ngamia wa Mwenyezi Mungu, mwacheni anywe maji fungu lake.
:14
Lakini walimkadhibisha na wakamchinja ngamia, kwa hivyo Mola wao Mlezi aliwaangamiza kwa sababu ya dhambi zao na akawafuta kabisa.
:15
Wala Yeye haogopi matokeo yake.