Maktaba yote ya Kiislamu

88 - The Overwhelming - Al-Ghāshiyah

:1

Je! Imekufikia khabari ya msiba wa kufudikiza?

:2

Siku hiyo nyuso zitainama,

:3

Zikifanya kazi, nazo taabani.

:4

Ziingie katika Moto unao waka -

:5

Zikinyweshwa kutoka chemchem inayo chemka.

:6

Hawatakuwa na chakula isipo kuwa kichungu chenye miba.

:7

Hakinenepeshi wala hakiondoi njaa.

:8

Siku hiyo nyuso nyengine zitakuwa kunjufu.

:9

Zitakuwa radhi kwa juhudi yao,

:10

Katika Bustani ya juu.

:11

Hawatasikia humo upuuzi.

:12

Humo imo chemchem inayo miminika.

:13

Humo vimo viti vilivyo nyanyuliwa,

:14

Na bilauri zilizo pangwa,

:15

Na matakia safu safu,

:16

Na mazulia yaliyo tandikwa.

:17

Je! Hawamtazami ngamia jinsi alivyo umbwa?

:18

Na mbingu jinsi ilivyo inuliwa?

:19

Na milima jinsi ilivyo thibitishwa?

:20

Na ardhi jinsi ilivyo tandazwa?

:21

Basi kumbusha! Hakika wewe ni Mkumbushaji.

:22

Wewe si mwenye kuwatawalia.

:23

Lakini anaye rudi nyuma na kukataa,

:24

Basi Mwenyezi Mungu atamuadhibu kwa adhabu iliyo kubwa kabisa!

:25

Hakika ni kwetu Sisi ndio marejeo yao.

:26

Kisha hakika ni juu yetu Sisi hisabu yao!