Maktaba yote ya Kiislamu

87 - The Most High - Al-'A`lá

:1

Litakase jina la Mola wako Mlezi aliye juu kabisa,

:2

Aliye umba, na akaweka sawa,

:3

Na ambaye amekadiria na akaongoa,

:4

Na aliye otesha malisho,

:5

Kisha akayafanya makavu, meusi.

:6

Tutakusomesha wala hutasahau,

:7

Ila akipenda Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye anayajua yaliyo dhaahiri na yaliyo fichikana.

:8

Na tutakusahilishia yawe mepesi.

:9

Basi kumbusha, kama kukumbusha kunafaa.

:10

Atakumbuka mwenye kuogopa.

:11

Na atajitenga mbali nayo mpotovu,

:12

Ambaye atauingia Moto mkubwa.

:13

Tena humo hatakufa wala hawi hai.

:14

Hakika amekwisha fanikiwa aliye jitakasa.

:15

Na akakumbuka jina la Mola wake Mlezi, na akasali.

:16

Lakini nyinyi mnakhiari maisha ya dunia!

:17

Na Akhera ni bora na yenye kudumu zaidi.

:18

Hakika haya yamo katika Vitabu vya mwanzo,

:19

Vitabu vya Ibrahimu na Musa.