87 - The Most High - Al-'A`lá
:1
Litakase jina la Mola wako Mlezi aliye juu kabisa,
:2
Aliye umba, na akaweka sawa,
:3
Na ambaye amekadiria na akaongoa,
:4
Na aliye otesha malisho,
:5
Kisha akayafanya makavu, meusi.
:6
Tutakusomesha wala hutasahau,
:7
Ila akipenda Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye anayajua yaliyo dhaahiri na yaliyo fichikana.
:8
Na tutakusahilishia yawe mepesi.
:9
Basi kumbusha, kama kukumbusha kunafaa.
:10
Atakumbuka mwenye kuogopa.
:11
Na atajitenga mbali nayo mpotovu,
:12
Ambaye atauingia Moto mkubwa.
:13
Tena humo hatakufa wala hawi hai.
:14
Hakika amekwisha fanikiwa aliye jitakasa.
:15
Na akakumbuka jina la Mola wake Mlezi, na akasali.
:16
Lakini nyinyi mnakhiari maisha ya dunia!
:17
Na Akhera ni bora na yenye kudumu zaidi.
:18
Hakika haya yamo katika Vitabu vya mwanzo,
:19
Vitabu vya Ibrahimu na Musa.