Maktaba yote ya Kiislamu

86 - The Nightcommer - Aţ-Ţāriq

:1

Naapa kwa mbingu na Kinacho kuja usiku!

:2

Na nini kitakacho kujuulisha ni nini hicho Kinacho kuja usiku?

:3

Ni Nyota yenye mwanga mkali.

:4

Hapana nafsi ila inayo mwangalizi.

:5

Hebu naajitazame mwanaadamu ameumbwa kwa kitu gani?

:6

Ameumbwa kwa maji yatokayo kwa kuchupa,

:7

Yatokayo baina ya mifupa ya mgongo na mbavu.

:8

Hakika Yeye ana uweza wa kumrudisha.

:9

Siku zitakapo dhihirishwa siri.

:10

Basi hatakuwa na nguvu wala msaidizi.

:11

Naapa kwa mbingu yenye marejeo!

:12

Na kwa ardhi inayo pasuka!

:13

Hakika hii ni kauli ya kupambanua.

:14

Wala si mzaha.

:15

Hakika wao wanapanga mpango.

:16

Na Mimi napanga mpango.

:17

Basi wape muhula makafiri - wape muhula pole pole.