Maktaba yote ya Kiislamu

85 - The Mansions of the Stars - Al-Burūj

:1

Naapa kwa mbingu yenye Buruji!

:2

Na kwa siku iliyo ahidiwa!

:3

Na kwa shahidi na kinacho shuhudiwa!

:4

Wameangamizwa watu wa makhandaki

:5

Yenye moto wenye kuni nyingi,

:6

Walipo kuwa wamekaa hapo,

:7

Na wao ni mashahidi wa yale waliyo kuwa wakiwafanyia Waumini.

:8

Nao hawakuona baya lolote kwao ila kuwa wakimuamini Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu, Msifiwa,

:9

Ambaye anao ufalme wa mbingu na ardhi; na Mwenyezi Mungu ni shaahidi wa kila kitu.

:10

Hakika walio wafitini Waumini wanaume na Waumini wanawake, kisha hawakutubu, basi watapata adhabu ya Jahannamu na watapata adhabu ya kuungua.

:11

Hakika walio amini na wakatenda mema watapata Bustani zenye mito ipitayo kati yake. Huko ndiko kufuzu kukubwa.

:12

Hakika kutesa kwa Mola wako Mlezi ni kukali.

:13

Yeye ndiye anaye anzisha na ndiye anaye rejeza tena,

:14

Naye ni Mwenye kusamehe, Mwenye mapenzi,

:15

Mwenye Kiti cha Enzi, Mtukufu,

:16

Atendaye ayatakayo.

:17

Je! Zimekuwasilia khabari za majeshi?

:18

Ya Firauni na Thamudi?

:19

Lakini walio kufuru wamo katika kukadhibisha.

:20

Na Mwenyezi Mungu nyuma yao amewazunguka.

:21

Bali hii ni Qur'ani tukufu

:22

Katika Ubao Ulio Hifadhiwa.