Maktaba yote ya Kiislamu

84 - The Sundering - Al-'Inshiqāq

:1

Itapo chanika mbingu,

:2

Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,

:3

Na ardhi itakapo tanuliwa,

:4

Na kuvitoa vilivyo kuwa ndani yake, ikawa tupu,

:5

Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,

:6

Ewe mtu! Hakika wewe unajikusuru kwa juhudi kumwendea Mola wako Mlezi, basi utamkuta.

:7

Ama atakaye pewa daftari lake kwa mkono wa kulia,

:8

Basi huyo atahisabiwa hisabu nyepesi,

:9

Na arudi kwa ahali zake na furaha.

:10

Na ama atakaye pewa daftari lake kwa nyuma ya mgongo wake,

:11

Basi huyo ataomba kuteketea.

:12

Na ataingia Motoni.

:13

Hakika alikuwa furahani kati ya jamaa zake.

:14

Huyo hakika alidhani kuwa hatarejea tena.

:15

Kwani? Hakika Mola wake Mlezi alikuwa akimwona!

:16

Basi ninaapa kwa wekundu wa jua linapo kuchwa,

:17

Na kwa usiku na unavyo vikusanya,

:18

Na kwa mwezi unapo pevuka,

:19

Lazima mtapanda t'abaka kwa t'abaka!

:20

Basi wana nini hawaamini?

:21

Na wanapo somewa Qur'ani hawasujudu?

:22

Bali walio kufuru wanakanusha tu.

:23

Na Mwenyezi Mungu anajua wanayo yadhamiria.

:24

Basi wabashirie adhabu chungu!

:25

Isipo kuwa wale walio amini na wakatenda mema; hao watakuwa na ujira usio malizika.