Maktaba yote ya Kiislamu

82 - The Cleaving - Al-'Infiţār

:1

Mbingu itapo chanika,

:2

Na nyota zitapo tawanyika,

:3

Na bahari zitakapo pasuliwa,

:4

Na makaburi yatapo fukuliwa,

:5

Hapo kila nafsi itajua ilicho tanguliza, na ilicho bakisha nyuma.

:6

Ewe mwanaadamu! Nini kilicho kughuri ukamwacha Mola wako Mlezi Mtukufu?

:7

Aliye kuumba, akakuweka sawa, akakunyoosha,

:8

Katika sura yoyote aliyo ipenda akakujenga.

:9

Sivyo hivyo! Bali nyinyi mnaikanusha Siku ya Malipo.

:10

Na hakika bila ya shaka wapo walinzi juu yenu,

:11

Waandishi wenye hishima,

:12

Wanayajua mnayo yatenda.

:13

Hakika wema bila ya shaka watakuwa katika neema,

:14

Na hakika waovu bila ya shaka watakuwa Motoni;

:15

Wataingia humo Siku ya Malipo.

:16

Na hawatoacha kuwamo humo.

:17

Na nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?

:18

Tena nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?

:19

Siku ambayo nafsi haitakuwa na madaraka yoyote juu ya nafsi; na amri yote siku hiyo ni ya Mwenyezi Mungu tu.