Maktaba yote ya Kiislamu

80 - He Frowned - `Abasa

:1

Alikunja kipaji na akageuka,

:2

Kwa sababu alimjia kipofu!

:3

Na nini kitakujuulisha pengine yeye atatakasika?

:4

Au atawaidhika, na mawaidha yamfae?

:5

Ama ajionaye hana haja,

:6

Wewe ndio unamshughulikia?

:7

Na si juu yako kama hakutakasika.

:8

Ama anaye kujia kwa juhudi,

:9

Naye anaogopa,

:10

Ndio wewe unampuuza?

:11

Sivyo hivyo! Huku ni kukumbushana.

:12

Basi anaye penda akumbuke.

:13

Yamo katika kurasa zilizo hishimiwa,

:14

Zilizo inuliwa, zilizo takaswa.

:15

Zimo mikononi mwa Malaika waandishi,

:16

Watukufu, wema.

:17

Ameangamia mwanaadamu! Nini kinacho mkufurisha?

:18

Kwa kitu gani amemuumba?

:19

Kwa tone la manii, akamuumba na akamkadiria.

:20

Kisha akamsahilishia njia.

:21

Kisha akamfisha, akamtia kaburini.

:22

Kisha apendapo atamfufua.

:23

La! Hajamaliza aliyo muamuru.

:24

Hebu mtu na atazame chakula chake.

:25

Hakika Sisi tumemimina maji kwa nguvu,

:26

Tena tukaipasua pasua ardhi kwa nguvu,

:27

Kisha tukaotesha humo nafaka,

:28

Na zabibu, na mimea ya majani,

:29

Na mizaituni, na mitende,

:30

Na bustani zenye miti iliyo songana baraabara,

:31

Na matunda, na malisho ya wanyama;

:32

Kwa manufaa yenu na mifugo yenu.

:33

Basi utakapo kuja ukelele,

:34

Siku ambayo mtu atamkimbia nduguye,

:35

Na mamaye na babaye,

:36

Na mkewe na wanawe -

:37

Kila mtu miongoni mwao siku hiyo atakuwa na lake la kumtosha.

:38

Siku hiyo ziko nyuso zitazo nawiri,

:39

Zitacheka, zitachangamka;

:40

Na nyuso siku hiyo zitakuwa na mavumbi,

:41

Giza totoro litazifunika,

:42

Hao ndio makafiri watenda maovu.