Maktaba yote ya Kiislamu

78 - The Tidings - An-Naba

:1

WANAULIZANA nini?

:2

Ile khabari kuu,

:3

Ambayo kwayo wanakhitalifiana.

:4

La! Karibu watakuja jua.

:5

Tena la! Karibu watakuja jua.

:6

Kwani hatukuifanya ardhi kama tandiko?

:7

Na milima kama vigingi?

:8

Na tukakuumbeni kwa jozi?

:9

Na tukakufanya kulala kwenu ni mapumziko?

:10

Na tukaufanya usiku ni nguo?

:11

Na tukaufanya mchana ni wa kuchumia maisha?

:12

Na tukajenga juu yenu saba zenye nguvu?

:13

Na tukaifanya taa yenye mwanga na joto;

:14

Na tukateremsha maji yanayo anguka kwa kasi kutoka mawinguni,

:15

Ili tutoe kwayo nafaka na mimea,

:16

Na mabustani yenye miti iliyo kamatana.

:17

Hakika siku ya uamuzi imewekewa wakati wake,

:18

Siku litapo pulizwa barugumu, nanyi mtakuja kwa makundi,

:19

Na mbingu zitafunguliwa, ziwe milango,

:20

Na milima itaondolewa na itakuwa kama sarabi.

:21

Hakika Jahannamu inangojea!

:22

Kwa walio asi ndio makaazi yao,

:23

Wakae humo karne baada ya karne,

:24

Hawataonja humo chochote kibaridi wala kinywaji,

:25

Ila maji yamoto sana na usaha,

:26

Ndio jaza muwafaka.

:27

Hakika hao hawakuwa wakitaraji kuwa kuna hisabu.

:28

Na wakikanusha Aya zetu kwa nguvu.

:29

Na kila kitu Sisi tumekidhibiti kwa kukiandika.

:30

Basi onjeni! Nasi hatutakuzidishieni ila adhabu!

:31

Hakika wachamngu wanastahiki kufuzu,

:32

Mabustani na mizabibu,

:33

Na wake walio lingana nao,

:34

Na bilauri zilizo jaa,

:35

Hawatasikia humo upuuzi wala uwongo -

:36

Malipo kutoka kwa Mola wako Mlezi, kipawa cha kutosha.

:37

Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilio baina yao, Arrahman, Mwingi wa rehema; hawamiliki usemi mbele yake!

:38

Siku atakapo simama Roho na Malaika kwa safu. Hawatasema ila Mwingi wa rehema aliye mruhusu, na atasema yaliyo sawa tu.

:39

Hiyo ndiyo Siku ya haki. Basi anaye taka na ashike njia arejee kwa Mola wake Mlezi.

:40

Hakika tumekuhadharisheni adhabu iliyo karibu kufika; Siku ambayo mtu atakapo ona yaliyo tangulizwa na mikono yake; na kafiri atasema: Laiti ningeli kuwa udongo!