Maktaba yote ya Kiislamu

77 - The Emissaries - Al-Mursalāt

:1

Naapa kwa zinazo tumwa kwa upole!

:2

Na zinazo vuma kwa kasi!

:3

Na zikaeneza maeneo yote!

:4

Na zinazo farikisha zikatawanya!

:5

Na zinazo peleka mawaidha!

:6

Kwa kuudhuru au kuonya,

:7

Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka yatakuwa!

:8

Wakati nyota zitakapo futwa,

:9

Na mbingu zitakapo pasuliwa,

:10

Na milima itakapo peperushwa,

:11

Na Mitume watakapo wekewa wakati wao,

:12

Kwa siku gani hiyo wamewekewa muda huo?

:13

Kwa siku ya kupambanua!

:14

Na nini kitakacho kujuulisha siku ya kupambanua ni nini?

:15

Ole wao, siku hiyo hao wanao kanusha!

:16

Kwani hatukuwaangamiza walio tangulia?

:17

Kisha tukawafuatilizia walio fuatia?

:18

Ndio kama hivi tuwatendavyo wakosefu!

:19

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

:20

Kwani hatukukuumbeni kwa maji ya kudharauliwa?

:21

Kisha tukayaweka mahali pa utulivu madhubuti?

:22

Mpaka muda maalumu?

:23

Tukakadiria na Sisi ni wabora wa kukadiria.

:24

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

:25

Kwani hatukuifanya ardhi yenye kukusanya

:26

Walio hai na maiti?

:27

Na ndani yake tukaweka milima mirefu yenye kuthibiti, na tunakunywesheni maji matamu?

:28

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

:29

Nendeni kwenye adhabu mliyo kuwa mkiikanusha!

:30

Nendeni kwenye kivuli chenye mapande matatu!

:31

Hakikingi moto, wala hakiwaepushi na mwako.

:32

Hakika Moto huo unatoa macheche kama majumba!

:33

Kama kwamba ni ngamia wa rangi ya manjano!

:34

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

:35

Hii ni siku ambayo hawatatamka kitu,

:36

Wala hawataruhusiwa kutoa udhuru.

:37

Ole wao siku hiyo hao walio kanusha!

:38

Hii ndiyo siku ya kupambanua. Tumekukusanyeni nyinyi na walio tangulia.

:39

Ikiwa mnayo hila, nifanyieni hila Mimi!

:40

Ole wao siku hiyo hao walio kanusha!

:41

Hakika wachamngu watakuwa katika vivuli na chemchem,

:42

Na matunda wanayo yapenda,

:43

Kuleni na kunyweni kwa furaha kwa yale mliyo kuwa mkiyatenda.

:44

Hakika ndio kama hivyo tunavyo walipa watendao mema.

:45

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

:46

Kuleni na mjifurahishe kidogo tu. Hakika nyinyi ni wakosefu!

:47

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

:48

Na wakiambiwa: Inameni! Hawainami.

:49

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

:50

Basi maneno gani baada ya haya watayaamini?