Maktaba yote ya Kiislamu

55 - The Beneficent - Ar-Raĥmān

:1

Arrah'man, Mwingi wa Rehema

:2

Amefundisha Qur'ani.

:3

Amemuumba mwanaadamu,

:4

Akamfundisha kubaini.

:5

Jua na mwezi huenda kwa hisabu.

:6

Na mimea yenye kutambaa, na miti, inanyenyekea.

:7

Na mbingu ameziinua, na ameweka mizani,

:8

Ili msidhulumu katika mizani.

:9

Na wekeni mizani kwa haki, wala msipunje katika mizani.

:10

Na ardhi ameiweka kwa ajili ya viumbe.

:11

Humo yamo matunda na mitende yenye mafumba.

:12

Na nafaka zenye makapi, na rehani.

:13

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha

:14

Amemuumba mtu kwa udongo wa kinamo..

:15

Na akawaumba majini kwa ulimi wa moto.

:16

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha

:17

Mola Mlezi wa mashariki mbili na wa magharibi mbili.

:18

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

:19

Anaziendesha bahari mbili zikutane;

:20

Baina yao kipo kizuizi, zisiingiliane.

:21

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

:22

Katika hizo bahari mbili zinatoka lulu na marijani.

:23

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

:24

Na ni vyake Yeye hivi viendavyo baharini vilivyo undwa kama vilima.

:25

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

:26

Kila kilioko juu yake kitatoweka.

:27

Na atabakia Mwenyewe Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu.

:28

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

:29

Vinamwomba Yeye vilivyomo katika mbingu na ardhi. Kila siku Yeye yumo katika mambo.

:30

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

:31

Tutakuhisabuni enyi makundi mawili.

:32

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

:33

Enyi makundi ya majini na watu! Mkiweza kupenya kwenye mbingu na ardhi, basi penyeni! Hamtapenya ila kwa kupewa madaraka.

:34

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

:35

Mtapelekewa muwako wa moto na shaba; wala hamtashinda.

:36

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

:37

Itakapo pasuka mbingu ikawa nyekundu kama mafuta.

:38

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

:39

Siku hiyo hataulizwa dhambi zake mtu wala jini.

:40

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

:41

Watajuulikana wakosefu kwa alama zao, basi watashikwa kwa nywele zao za utosini na kwa miguu.

:42

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

:43

Hii ndiyo Jahannamu ambayo wakosefu wakiikanusha.

:44

Watakuwa wakizunguka baina ya hiyo na maji ya moto yanayo chemka.

:45

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

:46

Na mwenye kuogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi atapata Bustani mbili.

:47

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

:48

Bustani zenye matawi yaliyo tanda.

:49

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

:50

Ndani yake zimo chemchem mbili zinazo pita.

:51

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

:52

Humo katika kila matunda zimo namna mbili.

:53

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

:54

Wawe wameegemea matandiko yenye bit'ana ya hariri nzito; na matunda ya Bustani hizo yapo karibu.

:55

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

:56

Humo watakuwamo wanawake watulizao macho yao; hajawagusa mtu kabla yao wala jini.

:57

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

:58

Kama kwamba wao ni yakuti na marijani.

:59

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha.

:60

Ati yaweza kuwa malipo ya ihsani ila ihsani?

:61

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

:62

Na zaidi ya hizo zipo Bustani nyengine mbili.

:63

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

:64

Za kijani kibivu.

:65

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

:66

Na chemchem mbili zinazo furika.

:67

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

:68

Imo humo miti ya matunda, na mitende na mikomamanga.

:69

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

:70

Humo wamo wanawake wema wazuri.

:71

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

:72

Wanawake wazuri wanao tawishwa katika makhema.

:73

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

:74

Hajawagusa mtu wala jini kabla yao.

:75

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

:76

Wameegemea juu ya matakia ya kijani na mazulia mazuri.

:77

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

:78

Limetukuka jina la Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu.