Maktaba yote ya Kiislamu

105 - The Elephant - Al-Fīl

:1

Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo watenda wale wenye tembo?

:2

Kwani hakujaalia vitimbi vyao kuharibika?

:3

Na akawapelekea ndege makundi kwa makundi,

:4

Wakiwatupia mawe ya udongo wa Motoni,

:5

Akawafanya kama majani yaliyo liwa!