104 - The Traducer - Al-Humazah
:1
Ole wake kila safihi, msengenyaji!
:2
Aliye kusanya mali na kuyahisabu.
:3
Anadhani ya kuwa mali yake yatambakisha milele!
:4
Hasha! Atavurumishwa katika H'ut'ama.
:5
Na nani atakujuvya ni nini H'ut'ama?
:6
Moto wa Mwenyezi Mungu ulio washwa.
:7
Ambao unapanda nyoyoni.
:8
Hakika huo utafungiwa nao
:9
Kwenye nguzo zilio nyooshwa.