Maktaba yote ya Kiislamu

104 - The Traducer - Al-Humazah

:1

Ole wake kila safihi, msengenyaji!

:2

Aliye kusanya mali na kuyahisabu.

:3

Anadhani ya kuwa mali yake yatambakisha milele!

:4

Hasha! Atavurumishwa katika H'ut'ama.

:5

Na nani atakujuvya ni nini H'ut'ama?

:6

Moto wa Mwenyezi Mungu ulio washwa.

:7

Ambao unapanda nyoyoni.

:8

Hakika huo utafungiwa nao

:9

Kwenye nguzo zilio nyooshwa.