1
Ole wake kila safihi, msengenyaji!
2
Aliye kusanya mali na kuyahisabu.
3
Anadhani ya kuwa mali yake yatambakisha milele!
4
Hasha! Atavurumishwa katika H'ut'ama.
5
Na nani atakujuvya ni nini H'ut'ama?
6
Moto wa Mwenyezi Mungu ulio washwa.
7
Ambao unapanda nyoyoni.
8
Hakika huo utafungiwa nao
9
Kwenye nguzo zilio nyooshwa.