Maktaba yote ya Kiislamu
1

Ole wake kila safihi, msengenyaji!

2

Aliye kusanya mali na kuyahisabu.

3

Anadhani ya kuwa mali yake yatambakisha milele!

4

Hasha! Atavurumishwa katika H'ut'ama.

5

Na nani atakujuvya ni nini H'ut'ama?

6

Moto wa Mwenyezi Mungu ulio washwa.

7

Ambao unapanda nyoyoni.

8

Hakika huo utafungiwa nao

9

Kwenye nguzo zilio nyooshwa.