Maktaba yote ya Kiislamu

101 - The Calamity - Al-Qāri`ah

:1

Inayo gonga!

:2

Nini Inayo gonga?

:3

Na nini kitacho kujuilisha nini Inayo gonga?

:4

Siku ambayo watu watakuwa kama nondo walio tawanyika;

:5

Na milima itakuwa kama sufi zilizo chambuliwa!

:6

Basi yule ambaye mizani yake itakuwa nzito,

:7

Huyo atakuwa katika maisha ya kupendeza.

:8

Na yule ambaye mizani yake itakuwa khafifu,

:9

Huyo maskani yake yatakuwa Moto wa Hawiya!

:10

Na nini kitacho kujuilisha nini hiyo?

:11

Ni Moto mkali!