101 - The Calamity - Al-Qāri`ah
:1
Inayo gonga!
:2
Nini Inayo gonga?
:3
Na nini kitacho kujuilisha nini Inayo gonga?
:4
Siku ambayo watu watakuwa kama nondo walio tawanyika;
:5
Na milima itakuwa kama sufi zilizo chambuliwa!
:6
Basi yule ambaye mizani yake itakuwa nzito,
:7
Huyo atakuwa katika maisha ya kupendeza.
:8
Na yule ambaye mizani yake itakuwa khafifu,
:9
Huyo maskani yake yatakuwa Moto wa Hawiya!
:10
Na nini kitacho kujuilisha nini hiyo?
:11
Ni Moto mkali!