Maktaba yote ya Kiislamu
1

Inayo gonga!

2

Nini Inayo gonga?

3

Na nini kitacho kujuilisha nini Inayo gonga?

4

Siku ambayo watu watakuwa kama nondo walio tawanyika;

5

Na milima itakuwa kama sufi zilizo chambuliwa!

6

Basi yule ambaye mizani yake itakuwa nzito,

7

Huyo atakuwa katika maisha ya kupendeza.

8

Na yule ambaye mizani yake itakuwa khafifu,

9

Huyo maskani yake yatakuwa Moto wa Hawiya!

10

Na nini kitacho kujuilisha nini hiyo?

11

Ni Moto mkali!