1
Kumekushughulisheni kutafuta wingi,
2
Mpaka mje makaburini!
3
Sivyo hivyo! Mtakuja jua!
4
Tena sivyo hivyo! Mtakuja jua!
5
Sivyo hivyo! Lau mngeli jua kwa ujuzi wa yakini,
6
Basi bila ya shaka mtaiona Jahannamu!
7
Tena, bila ya shaka, mtaiona kwa jicho la yakini.
8
Tena bila ya shaka mtaulizwa siku hiyo juu ya neema.