Maktaba yote ya Kiislamu

100 - The Courser - Al-`Ādiyāt

:1

Naapa kwa farasi wendao mbio wakipumua,

:2

Na wakitoa moto kwa kupiga kwato zao chini,

:3

Wakishambulia wakati wa asubuhi,

:4

Huku wakitimua vumbi,

:5

Na wakijitoma kati ya kundi,

:6

Hakika mwanaadamu ni mtovu wa fadhila kwa Mola wake Mlezi!

:7

Na hakika yeye mwenyewe bila ya shaka ni shahidi wa hayo!

:8

Naye hakika bila ya shaka ana nguvu za kupenda mali!

:9

Kwani hajui watakapo fufuliwa waliomo makaburini?

:10

Na yakakusanywa yaliomo vifuani?

:11

Kuwa hakika Mola wao Mlezi siku hiyo bila ya shaka atakuwa na khabari zao wote!