100 - The Courser - Al-`Ādiyāt
:1
Naapa kwa farasi wendao mbio wakipumua,
:2
Na wakitoa moto kwa kupiga kwato zao chini,
:3
Wakishambulia wakati wa asubuhi,
:4
Huku wakitimua vumbi,
:5
Na wakijitoma kati ya kundi,
:6
Hakika mwanaadamu ni mtovu wa fadhila kwa Mola wake Mlezi!
:7
Na hakika yeye mwenyewe bila ya shaka ni shahidi wa hayo!
:8
Naye hakika bila ya shaka ana nguvu za kupenda mali!
:9
Kwani hajui watakapo fufuliwa waliomo makaburini?
:10
Na yakakusanywa yaliomo vifuani?
:11
Kuwa hakika Mola wao Mlezi siku hiyo bila ya shaka atakuwa na khabari zao wote!