Maktaba yote ya Kiislamu
1

Naapa kwa farasi wendao mbio wakipumua,

2

Na wakitoa moto kwa kupiga kwato zao chini,

3

Wakishambulia wakati wa asubuhi,

4

Huku wakitimua vumbi,

5

Na wakijitoma kati ya kundi,

6

Hakika mwanaadamu ni mtovu wa fadhila kwa Mola wake Mlezi!

7

Na hakika yeye mwenyewe bila ya shaka ni shahidi wa hayo!

8

Naye hakika bila ya shaka ana nguvu za kupenda mali!

9

Kwani hajui watakapo fufuliwa waliomo makaburini?

10

Na yakakusanywa yaliomo vifuani?

11

Kuwa hakika Mola wao Mlezi siku hiyo bila ya shaka atakuwa na khabari zao wote!