Maktaba yote ya Kiislamu
1

Itakapo tetemeshwa ardhi kwa mtetemeko wake!

2

Na itakapo toa ardhi mizigo yake!

3

Na mtu akasema: Ina nini?

4

Siku hiyo itahadithia khabari zake.

5

Kwa sababu Mola wake Mlezi ameifunulia!

6

Siku hiyo watu watatoka kwa mfarakano wakaonyweshwe vitendo vyao!

7

Basi anaye tenda chembe ya wema, atauona!

8

Na anaye tenda chembe ya uovu atauona!