1
Itakapo tetemeshwa ardhi kwa mtetemeko wake!
2
Na itakapo toa ardhi mizigo yake!
3
Na mtu akasema: Ina nini?
4
Siku hiyo itahadithia khabari zake.
5
Kwa sababu Mola wake Mlezi ameifunulia!
6
Siku hiyo watu watatoka kwa mfarakano wakaonyweshwe vitendo vyao!
7
Basi anaye tenda chembe ya wema, atauona!
8
Na anaye tenda chembe ya uovu atauona!