99 - The Earthquake - Az-Zalzalah
:1
Itakapo tetemeshwa ardhi kwa mtetemeko wake!
:2
Na itakapo toa ardhi mizigo yake!
:3
Na mtu akasema: Ina nini?
:4
Siku hiyo itahadithia khabari zake.
:5
Kwa sababu Mola wake Mlezi ameifunulia!
:6
Siku hiyo watu watatoka kwa mfarakano wakaonyweshwe vitendo vyao!
:7
Basi anaye tenda chembe ya wema, atauona!
:8
Na anaye tenda chembe ya uovu atauona!