Maktaba yote ya Kiislamu

99 - The Earthquake - Az-Zalzalah

:1

Itakapo tetemeshwa ardhi kwa mtetemeko wake!

:2

Na itakapo toa ardhi mizigo yake!

:3

Na mtu akasema: Ina nini?

:4

Siku hiyo itahadithia khabari zake.

:5

Kwa sababu Mola wake Mlezi ameifunulia!

:6

Siku hiyo watu watatoka kwa mfarakano wakaonyweshwe vitendo vyao!

:7

Basi anaye tenda chembe ya wema, atauona!

:8

Na anaye tenda chembe ya uovu atauona!