Maktaba yote ya Kiislamu

75 - The Resurrection - Al-Qiyāmah

:1

Ninaapa kwa Siku ya Kiyama!

:2

Na ninaapa kwa nafsi inayo jilaumu!

:3

Anadhani mtu kuwa Sisi hatutaikusanya mifupa yake?

:4

Kwani! Sisi tunaweza hata kuziweka sawa sawa ncha za vidole vyake!

:5

Lakini mtu anataka tu kuendelea na maasi kwa siku zilioko mbele yake.

:6

Anauliza: Lini itakuwa hiyo Siku ya Kiyama?

:7

Basi jicho litapo dawaa,

:8

Na mwezi utapo patwa,

:9

Na likakusanywa jua na mwezi,

:10

Siku hiyo mtu atasema: Yako wapi makimbilio?

:11

La! Hapana pa kukimbilia!

:12

Siku hiyo pa kutua ni kwa Mola wako Mlezi tu.

:13

Siku hiyo ataambiwa aliyo yatanguliza na aliyo yaakhirisha.

:14

Bali mtu ni hoja juu ya nafsi yake.

:15

Na ingawa atatoa chungu ya udhuru.

:16

Usiutikisie huu wahyi ulimi wako kwa kuufanyia haraka.

:17

Hakika ni juu yetu kuukusanya na kuusomesha.

:18

Tunapo usoma, basi nawe fuatiliza kusoma kwake.

:19

Kisha ni juu yetu kuubainisha.

:20

Hasha! Bali nyinyi mnapenda maisha ya duniani,

:21

Na mnaacha maisha ya Akhera.

:22

Zipo nyuso siku hiyo zitao ng'ara,

:23

Zinamwangallia Mola wao Mlezi.

:24

Na zipo nyuso siku hiyo zitakao kunjana.

:25

Zitajua ya kuwa zitafikiwa na livunjalo uti wa mgongo.

:26

La, hasha! (Roho) itakapo fikia kwenye mafupa ya koo,

:27

Na pakasemwa: Nani wa kumganga?

:28

Na mwenyewe akajua kwa hakika kuwa huko ndiko kufariki;

:29

Na utapo ambatishwa muundi kwa muundi,

:30

Siku hiyo ndiyo kuchungwa kupelekwa kwa Mola wako Mlezi!

:31

Kwa sababu hakusadiki, wala hakusali.

:32

Bali alikanusha, na akageuka.

:33

Kisha akenda kwa ahali zake kwa matao.

:34

Ole wako, ole wako!

:35

Kisha Ole wako, ole wako!

:36

Ati anadhani binaadamu kuwa ataachwa bure?

:37

Kwani hakuwa yeye tone ya manii lilio shushwa?

:38

Kisha akawa kidonge cha damu, tena Mwenyezi Mungu akamuumba na akamtengeneza vilivyo.

:39

Kisha akamfanya namna mbili, mwanamume na mwanamke.

:40

Je! Huyo hakuwa ni Muweza wa kufufua wafu?