Maktaba yote ya Kiislamu

111 - The Palm Fiber - Al-Masad

:1

Imeangamia mikono ya Abu Lahab, na yeye pia ameangamia.

:2

Hayatamfaa mali yake, wala alivyo vichuma.

:3

Atauingia Moto wenye mwako.

:4

Na mkewe, mchukuzi wa kuni,

:5

Shingoni mwake iko kamba iliyo sokotwa.