Maktaba yote ya Kiislamu

110 - The Divine Support - An-Naşr

:1

Itakapo kuja nusura ya Mwenyezi Mungu na ushindi,

:2

Na ukaona watu wanaingia katika Dini ya Mwenyezi Mungu kwa makundi,

:3

Zitakase sifa za Mola wako Mlezi, na umwombe msamaha; hakika Yeye ndiye anaye pokea toba.