Maktaba yote ya Kiislamu
1

Je! Umemwona anaye kadhibisha Malipo?

2

Huyo ndiye anaye msukuma yatima,

3

Wala hahimizi kumlisha masikini.

4

Basi, ole wao wanao sali,

5

Ambao wanapuuza Sala zao;

6

Ambao wanajionyesha,

7

Nao huku wanazuia msaada.